Waziri mkuu wa Israel Bw. Benjamin Netanyahu jana alikutana na mshauri mwandamizi wa rais Donald Trump wa Marekani kuhusu masuala ya mashariki ya kati Bw. Jared Kushner, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Marekani kurejesha mazungumzo ya amani kati ya Israel na Palestina. Taarifa iliyotolewa na ikulu ya Marekani inasema Bw. Kushner alitumwa kwenye kanda hiyo kutimiza ahadi ya rais Trump ya kuleta "makubaliano ya mwisho" kati ya Israeli na Palestina.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |