Waziri mkuu wa Uingereza Bi. Theresa May alitoa taarifa jana, akiwaomba radhi wahanga wa ajali kubwa ya moto iliyotokea hivi karibuni kwenye jengo moja la makazi lenye ghorofa 24 magharibi mwa London, na kusababisha vifo vya watu wapatao 80. Bibi May amekiri kuwa hatua alizochukua wakati janga hilo hazikutosha, na serikali yake ilishindwa kuwasaidia wananchi wakati walipohitaji msaada. Bibi May pia amesema anafanya juhudi zote kushughulikia vizuri mambo baada ya janga hilo, na kwamba familia zote zilizopoteza nyumba katika ajali hiyo watapewa makazi ndani ya wiki tatu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |