Baraza la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa hivi karibuni lilipitisha azimio lililotolewa na China kuhusu mchango wa maendeleo katika kutimiza haki za binadamu, ambalo limepongezwa na kuungwa mkono na nchi zinazoendelea. Nchi hizo zinaona azimio hilo limeonesha matakwa ya nchi zinazoendelea, kuhimiza mshikamano kati ya nchi hizo, kuongeza ushawishi wa nchi zinazoendelea kwenye masuala ya haki za binadamu kwenye jumuiya ya kimataifa, na pia litatoa mwelekeo sahihi wa maendeleo ya Baraza la haki za binadamu. Nchi nyingi zinazoendelea zinalitaja azimio hilo kama "Ushindi kwenye masuala ya haki za binadamu".
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |