Katibu mkuu wa Jumuiya ya kujihami ya nchi za magharibi NATO Bw. Jens Stoltenberg amesema bajeti ya ulinzi ya jumuiya hiyo inatarajiwa kuongezeka kwa asilimia 4.3 mwaka huu, ikiwa ni mwaka wa tatu mfululizo kwa jumuiya hiyo kuongeza bajeti hiyo. Pia amesema mawaziri wa ulinzi wa nchi wanachama wa NATO watakutana leo kujadili utekelezaji wa maamuzi kuhusu ugawaji wa majukumu na mapambano dhidi ya ugaidi yaliyofikiwa kwenye mkutano wa kilele wa NATO uliofanyika mwezi Mei.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |