Wafanyabiashara na wakulima wa zao la kahawa watafaidi matunda ya kazi yao baada ya mashine ya kusindika bidhaa hiyo kununuliwa.
Akizungumzia ujio wa mashine hizo leo katika maonyesho ya Biashara ya Sabasaba, Meneja wa Shirika la Viwanda Vidogo Vidogo (Sido) Tawi la Mbeya, Cosmas Kinasa amesema kuwa wakulima wa zao hilo watasindika bidhaa zao wenyewe.
Amesema mashine hiyo ina uwezo wa kusaga kilo 300 za kahawa kwa saa.
Amesema lengo ni kumuinua mkulima mdogo na mfanyabiashara wa kati ambaye badala ya kusafirisha bidhaa hiyo kama malighafi ataiongezea ubora kwa kuisindika kabisa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |