Mjumbe maalumu wa serikali ya China anayeshughulikia masuala ya Afrika Bw. Xu Jinghu amekamilisha ziara ya siku tatu iliyoanza Jumanne nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo, ambako kwa nyakati tofauti alikutana na rais Joseph Kabila na naibu waziri mkuu wa nchi hiyo Bw. Leonard Okitundu. Bw. Xu Jinghu amesema China itaendelea kuunga mkono maendeleo ya DRC, kuimarisha ushirikiano wa kunufaishana kwenye sekta za miundombinu, nishati na utamaduni, na kutia nguvu mpya kwenye uhusiano wa wenzi wa kimkakati kati ya China na DRC.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |