Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Bw. António Guterres ametoa taarifa kupitia msemaji wake, akiipongeza tume ya kulinda amani ya Umoja wa Mataifa nchini Côte d'Ivoire UNOCI kwa kukamilisha majukumu yake, na kusema Umoja wa mataifa utaendelea kutoa uungaji mkono kwa Côte d'Ivoire. Kwenye taarifa hiyo Bw. Guterres pia amesifu juhudi za serikali ya Côte d'Ivoire na watu wake kwa ajili ya kukomesha msukosuko na kusukuma mbele mchakato wa amani nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |