Rais Petro Poroshenko wa Ukraine amesema washukiwa wanaotuhumiwa kutungua ndege ya abiria ya Malaysia MH17 mwezi Julai mwaka 2014 kwenye anga ya Ukraine watapandishwa kizimbani nchini Uholanzi. Rais Poroshenko aliandika kwenye ukurasa wake wa Facebook kwamba uamuzi wa kuchunguza kesi hiyo chini ya sheria za Uholanzi ulipitishwa na Timu ya pamoja ya uchunguzi, inayoundwa na wajumbe kutoka Uholanzi, Australia, Malaysia, Ubelgiji na Ukraine.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |