Nahodha wa zamani wa timu ya taifa ya Afrika kusini Bafana bafana, Steven Pienaar, amerejea nchini mwake na kujiunga na timu ya Bidwest Wits kwa mkataba wa mwaka mmoja. Pienaar mwenye umri wa miaka 35 amejiunga na timu hiyo baada ya kumaliza mkataba wake na klabu ya Sunderland ya nchini England.
Kiungo huyu amecheza soka ya kulipwa barani ulaya kwa miaka 16 akicheza soka katika nchi za Uholanzi, Ujerumani na England,.
Baadhi ya vilabu alivyochezea mchezaji huyu ni Ajax, Everton, Borussia Dortmund, Tottenham Hotspur na Sunderland
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |