Bunge la Ufaransa limepitisha uamuzi wa kurefusha kipindi cha hali ya dharura hadi Novemba 1 mwaka huu, ikiwa ni mara ya sita kwa nchi hiyo kuongeza muda hali ya dharura baada ya mashambulizi ya kigaidi yaliyotokea mwezi Novemba mwaka 2015 mjini Paris. Waziri wa mambo ya ndani wa Ufaransa Gerard Collomb amesema kudumisha hali ya dharura kunasaidia kuimarisha mapambano dhidi ya ugaidi nchini Ufaransa, na mwaka huu Ufaransa imezuia majaribio 7 ya mashambulizi ya kigaidi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |