Kupitia kwa wakili wake, Malinzi amewaandikia barua FIFA kuwataarifu kujitoa kwenye kamati hiyo kutokana na kuwa mikononi mwa sheria kwa sasa.
Malinzi pamoja na katibu wa TFF, Selestine Mwesigwa na mhasibu Nsiande Isawafo Mwanga wapo rumande hadi Julai 17, upelelezi wa kesi yao utakapokamilika baada ya kunyimwa dhamana Julai 3 katika kesi inayowakabili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |