Mkutano wa 26 wa Jumuiya ya usalama na ushirikiano barani Ulaya OSCE uliofungwa jana huko Minsk, Belarus, umepitisha taarifa ya Minsk inayotoa mwito kwa nchi wanachama kutekeleza diplomasia ya pande nyingi ili kuhakikisha usalama. Taarifa hiyo imetoa mapendekezo kwa serikali na mabunge ya nchi wanachama, kukabiliana na changamoto na matishio yanayoendelea kuongezeka. Mbali na hayo, mkutano huo pia umezitaka nchi wanachama kufanya juhudi za kutatua masuala ya kiuchumi na kimazingira, na kuhimiza mafungamano ya kikanda.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |