• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • IOC kutoa vibali vya olimpiki mwaka wa 2024 na 2028

    (GMT+08:00) 2017-07-13 09:21:10
    Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki IOC ilipiga kura Jumanne na kupitisha hoja ya kutoa vibali vya michuano ya Olimpiki vya mwaka 2024 na 2028 kwa mara moja.

    Wanachama wote 83 wa kamati hiyo waliokutana kwa kikao cha 130, walipiga kura kuunga mkono uamuzi uliofanywa na bodi ya IOC mwezi uliopita.

    Miji ya Los Angeles and Paris yalikuwa wawaniaji pekee walioweka maombi ya kuandaa michezo ya Olimpiki mwaka wa 2024 baada ya miji kadhaa zikiwemo Oslo, Roma, Budapest na Munich kujiondoa.

    Mwenyeji wa michezo hiyo ataamuliwa kwa kura itakayofanyika septemba 13 kwenye mji wa Lima nchini Peru, kwenye kikao cha 131 cha IOC.

    Meya wa Los Angeles Eric Garcetti na mwenzake wa Paris Anne Hildago waliungana jukwaani na kushikana mikono wakiwa pamoja na rais wa IOC Thomas Bach kwa ishara ya umoja na kusherehekea uamuzi huo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako