• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Senegal kuvaana na Kenya mechi za Africa Gold Cup

    (GMT+08:00) 2017-07-13 10:39:48
    TIMU ya taifa ya raga ya wachezaji 15 kila upande ya Senegal itawasili Kenya leo tayari kwa mashindano ya Africa Gold Cup Senegal inatarajiwa kushiriki mechi yake ya nne ya kombe hilo dhidi ya Kenya uwanjani RFUEA jijini Nairobi siku ya Jumamosi. Timu hiyo kutoka Afrika Magharibi inashikilia nafasi ya tano kwenye mashindano haya ya mataifa sita. Katika kombe hili, Kenya ni ya pili nyuma ya Namibia. Timu hiyo maarufu kama Simbas inawinda ushindi wa pili mfululizo dhidi ya Senegal baada ya kuichabanga zilipokutana mara ya kwanza mwaka 2009 katika Kombe la Afrika
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako