Tanzania inatarajiwa kufungua bustani yake ya kwanza ya kijiolojia ya Ngorongoro-Lengai yenye volkano hai. Ofisa mahusiano wa mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro Bw. Nickson Nyange amesema bustani hiyo yenye eneo la kilomita za mraba elfu 12 itahusisha volkano hai ya Lengai, ambayo ni kilele cha tatu cha juu zaidi nchini Tanzania, na inatarajiwa kuwa moja ya vivutio vikubwa kwenye bustani hiyo. Lakini mwanajiofizikia Sarah Stamps anayefanya utafiti kuhusu volkano hiyo alisema volkano hiyo inaweza kulipuka ndani ya wiki kadhaa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |