Waziri Mkuu pia amesema kuwa kuwepo kwa viwanda vya nguo kutasaidia wakulima wa pamba kuwa na soko.
Pia amewataka kupanda pamba kwa wingi ili sekta ya nguo iweze kupata malighafi ya kutosha.
Majaliwa alisema haya siku ya Jumamosi wakati alipotembelea kampuni ya Namera Group of Industries, ambayo inahusika katika kutengeneza bidhaa za nguo.
Majaliwa amesema viwanda vya nguo nchini ni hatua ya kumaliza matumizi ya nguo za mtumba, kwa sababu aina mbalimbali za nguo zinzotengezwa nchini bei yake itakuwa nafuu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |