• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kampuni ya teknolojia ya China yaeleza mradi wa uchunguzi wa dunia nchini Namibia

    (GMT+08:00) 2017-07-18 20:10:43

    Ujumbe kutoka kampuni ya teknolojia ya Tencent ya China umewasili mjini Windhoek, Namibia ili kutoa maelezo kuhusu mradi wake wa uchunguzi wa dunia, QQ Project X, utakaofanyika ijumaa wiki hii.

    Namibia imechaguliwa kuwa moja ya nchi mbili katika mradi huo kwa mwaka huu, ambapo wachunguzi watatembelea nchi hiyo na kubadilishana uzoefu wao kuhusu mtandao wa Internet.

    Wizara ya habari na teknolojia ya Namibia imesema, vijana 15 wanaojitolea kutoka China watakwenda nchini Namibia, na watapiga filamu za anga wakati wa usiku ambazo zitaonyeshwa baadaye kwenye mtandao wa Internet.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako