Timu ya mpira wa kikapu ya wanaume ya Uganda maarufu "Silverbacks", itashiriki kwa mara ya pili mfululizo katika mashindano ya mabingwa wa bara la Afrika AfroBasket mwezi septemba.
kocha wa Silverbacks Mandy Juruni anasema timu hiyo inataka kuboresha matokeo yake wakati huu kando na ilivyofanya msimu uliopita.
Timu hiyo ya vikapu imewekwa katika kundi moja na Angola, Morocco na Jamhuri ya Afrika ya Kati katika ndoo iliofanyika nchini Mauritius.
Kocha wa Silverbacks anasema mashindano hayo yanaipa timu yake nafasi ya kucheza tena na kuonyesha ubabe wao katika mchezo huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |