Tume ya uchaguzi ya India imetangaza kuwa Ram Nath Kovind kutoka chama cha NDA ameshinda kwenye uchaguzi mkuu kwa kupata asilimia 65 za kura, na kuwa rais mpya wa India. Bw. Kovind mwenye umri wa miaka 71 aliwahi kufanya kazi katika mahakama ya juu ya mji wa Delhi na mahakama kuu ya India kwa miaka 15. Kuanzia mwaka 1994 hadi 2006, alikuwa seneta wa bunge la India, na mwaka 2015 aliteuliwa kuwa gavana wa jimbo la Bihar.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |