Kenya imepata ushindi mara tatu kwa mpigo baada ya kuilemaza Benin katika mashindano yanayoendelea ya Davis CUP Africa Zone jijini Cairo.
Ushindi huo umeimarisha nafasi ya Kenya katika Pool B baada ya kushinda mechi tatu na kuiweka timu hiyo kwa nafasi nzuri kuingia nusu fainali ya mashindano hayo.
Hii pia ilikuwa kisasi kitamu kwa Wakenya, ambao walipoteza kwa Benin katika hatua hiyo wakati wa mashindano ya mwaka jana yaliyofanyika nchini Madagascar.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |