Jeshi la Iraq limesema kuwa jeshi la anga la Iraq lilifanya shambulizi kutoka anga dhidi ya wilaya mbili za mkoa wa Al Anbar na kuwaua wapiganaji zaidi ya 10 wa kundi la Islamic State.
Idara ya uongozaji ya kampeni ya pamoja ya Iraq ilitoa taarifa ikisema kuwa ndege za vita za jeshi la anga la Iraq zilifanya mashambulizi na kuvunja makao makuu ya uongozaji, ghala mbili za silaha na kiwanda cha kutengeneza mabomu ya gari, na kuwaua wapiganaji zaidiya 10 wa kundi hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |