Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amezindua uwanja wa ndege wa kimataifa wa Isiolo, kaskazini mashariki mwa nchi hiyo, ambao umetajwa kuwa utasaidia kuhimiza maendeleo ya utalii na uchumi kwenye maeneo ya kaskazini ya nchi hiyo. Uwanja huo ambao ni sehemu ya mradi wa ushoroba wa usafirishaji kutoka bandari ya Lamu, kupitia Sudan Kusini hadi Ethiopia LAPSSET, ni uwanja wa tano wa kimataifa nchini Kenya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |