Jeshi la Misri limesema, wapiganaji 40 wameuawa katika operesheni ya kijeshi iliyofanyika mkoa wa Sinai Kaskazini.
Kwenye taarifa yake msemaji wa jeshi hilo Bw. Tamer el Refai amesema, jeshi hilo limewaua wapiganaji hatari zaidi 40 katika operesheni ya ardhini na angani katika miji ya Arish, Rafah na Sheikh Zuweid mkoani Sinai Kaskazini.
Ameongeza kuwa watuhumiwa wengine watano wamekamatwa katika operesheni hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |