Vyombo vya habari vya Nigeria vimeripoti kuwa shambulizi hilo lilitokea karibu na eneo la bonde la Ziwa Chad wakati kikundi hicho kilipotafuta mafuta chini ya ulinzi wa jeshi la Nigeria na makundi yenye silaha ya umma.
Baada ya shambulizi hilo, serikali ya Nigeria ilisimamisha mara moja kazi zote za utafutaji mafuta kwenye eneo hilo. Hivi karibuni, jeshi la Nigeria liliwahi kutangaza kuwa litamkamata kiongozi wa kundi la Boko Haram Abubakar Shekau ndani ya siku 40. Hata hivyo bado haijulikani kama shambulizi hilo linahusiana na tangazo hilo la jeshi la Nigeria au la.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |