Wafanyakazi wa maduka ya Nakumatt nchini Kenya wamegoma Jumanne wakilalamikia kutolipwa mishahara yao na mazingira duni ya kazi.
Maduka hayo ya nakumattt yamekuwa na shinikizo kubwa huku yakikabiliwa na deni la zaidi ya shilingi bilioni 17.
Mjini Nairobi wafanyakazi hao walifanya maandamano katikati mwa jiji wakibeba mabango kuelezea malalamishi yao.
Aidha kumekuwa na maandamano sawa na hayo mjini Kisumu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |