• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Wakenya 3 wafuzu kwa fainali ya mbio za mita 3000 kurura viunzi na maji

    (GMT+08:00) 2017-08-07 10:39:23
    Kenya imejiongezea nafasi ya kujipatia medali zote katika mbio za mita 3000 kuruka viunzi na maji kama ilivyo desturi baada ya nyota wake kufuzu mchujo na kuingia fainali siku ya jumapili.

    Katika mchujo wa kwanza Jirus Birech alimaliza katika nafasi ya tano na kufuzu kwa fainali. Birech alitumia muda wa dakika 8 sekunde 23 nukta 84.

    Soufiane Elbakkali kutoka Morocco aliibuka mshindi katika mchujo huu kwa kuweka muda wa dakika 8 sekunde 22 nukta 60.

    Mchujo wa pili bingwa mtetezi Ezekiel Kemboi ambaye pia ni bingwa mara nne wa dunia alimaliza katika nafasi ya nne na kufuzu kwa fainali.

    Bingwa wa michezo ya Olimpiki na mshindi wa fedha katika mashindano ya dunia Conseslus Kipruto alimaliza wa kwanza katika mchujo wa tatu na kufuzu moja kwa moja katika fainali.

    Aliyekuwa bingwa wa Olimpiki na vile vile bingwa wa mwaka 2017 Brimin Kipruto hakufanikiwa kufuzu kwa fainali kwani alimaliza katika nafasi ya saba katika mchujo wa tatu. Fainali ya mbio hizi itafanyika siku ya Jumanne.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako