Bodi mpya za wakurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo ya Kahawa Uganda (UCDA) zimepewa kazi ya kuboresha mauzo ya kahawa ili kuwezesha nchi kufikia lengo lake la kuuza nje mifuko milioni 20 ya kahawa ifikapo mwaka 2020.
Waziri wa kilimo Christopher Kibanzanga aliwahimiza wakurungenzi hao kukuza uzalishaji kwa kuwa ni moja ya mazao yaliyopewa kipaumbele ili kuimarisha kipato cha kati cha nchi.
Katika mwaka wa fedha wa 2016/17, Uganda ilipata zaidi ya dola milioni 489 kutoka kwa mauzo ya nje ya mifuko milioni 4.2.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |