Leo ni kumbukumbu ya miaka 72 tangu Japan ikubali kushindwa katika Vita Kuu ya Pili ya Dunia.
Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Bibi Hua Chunying amesema, jeshi la Japan lililoivamia China katika Vita Kuu ya Pili ya Dunia lilifanya uhalifu mkubwa dhidi ya binadamu. Historia hii yenye mashahidi thabiti haiwezi kukanushwa. Amesema China inaitarajia Japan iwe na mtazamo sahihi na kuitafakari kwa kina historia ya uvamizi, na kuheshimu kihalisi hisia za wananchi wa nchi za Asia zilizovamiwa ikiwemo China.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |