Uamuzi huo umetangazwa leo Jumanne na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Jodarn Rugimbana wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini hapa.
Jodarn amesema wanatenga eneo hilo lenye ukubwa wa ekari 400 kwa ajili ya viwanda na litakalobakia litatengenezwa uwe uwanja wa kimataifa.
Amesema katika maonyesho yaliyomalizika wiki iliyopita ambayo yamesimamiwa na mkoa baada ya kuondolewa kwenye usimamizi wa Chama cha wakulima (Taso) wamefanikiwa kukusanya Sh 226 milioni.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |