Polisi nchini Uholanzi wanachunguza tishio la usalama mjini Rotterdam baada ya gari moja lenye mitungi ya gesi kuzuiwa na dereva wake kukamatwa karibu na jumba la maonesho mjini humo. Polisi wamesema gari hilo lililosajiliwa nchini Hispania lilizuiwa saa tatu hadi nne jana usiku, na dereva alikamatwa na kupelekwa kwenye kituo cha polisi kwa ajili ya uchunguzi. Baada ya tukio hilo, maonesho ya muziki yaliyopangwa kufanyika kwenye jumba hilo yalifutwa na watu waliokuwa kwenye jengo hilo waliondolewa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |