• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Jumuiya ya wanamazingira ya Afrika yaipongeza Kenya kupiga marufuku mifuko ya plastiki

    (GMT+08:00) 2017-08-29 09:30:37

    Jumuiya ya Greenpeace Africa imeipongeza serikali ya Kenya kwa kupiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki, na kusema hiyo ni hatua kubwa ya kufikia hali endelevu ya mazingira.

    Mkurugenzi mtendaji wa Greenpeace Africa Bibi Njeri Kabeberi amesema hatua hiyo ya serikali ya Kenya imezitia moyo nchi nyingine za Afrika, kupiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki ambayo ni tishio kwa mfumo wa viumbe na maisha.

    Mwezi Februari mwaka huu waziri wa mazingira na maliasili wa Kenya Bibi Judy Wakhungu alitangaza uamuzi wa serikali kupiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki. Lakini marufuku hiyo ilizuiwa mahakamani na wazalishaji wa mifuko hiyo, hadi kutakapokuwa na njia mbadala. Wikiendi iliyopita mahakama ilitoa uamuzi tena kuruhusu marufuku ya mifuko hiyo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako