Wizara ya afya ya Burundi imesema, maambukizi 24 ya ugonjwa wa kipindipindi yameripotiwa kwenye eneo la Nyanza-Lac katika jimbo la Makamba, kusini magharibi mwa nchi hiyo ndani ya wiki mbili zilizopita. Msemaji wa wizara hiyo Bw. Thaddee Ndikumana amesema kati ya wagonjwa hao 24, 21 wameruhusiwa kuondoka hospitali na wengine watatu bado wanaendelea kupewa matibabu. Bw. Ndikumana amewataka wakazi wa eneo hilo wafuate kanuni za usafi na kuchemsha maji ya kunywa na kutumia vyoo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |