• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Duru ya tatu ya mazungumzo ya Brexit haikuwa na mafanikio

    (GMT+08:00) 2017-09-01 09:20:47

    Duru ya tatu ya mazungumzo kuhusu Uingereza kujitoa Umoja wa Ulaya iliyomalizika jana mjini Brussels, haikuwa na mafanikio kutokana na maoni tofauti.

    Mjumbe mwandamizi wa Umoja wa Ulaya kwenye mazungumzo hayo Bw. Michel Barnier amesema kuna tofauti kubwa kwenye haki za wakazi wa umoja wa Ulaya na gharama zinazotakiwa kulipwa na Uingereza kujitoa Umoja wa Ulaya. Kutokana na hali hii, hawezi kupendekeza Baraza la Ulaya kufanya majadiliano kuhusu uhusiano kati ya pande hizo mbili katika siku za baadaye.

    Lakini waziri wa Uingereza anayeshughulikia Uingereza kujitoa Umoja wa Ulaya Bw. David Davis amesisitiza kuwa, masuala ya kujitoa Umoja wa Ulaya na uhusiano kati ya pande hizo mbili yanapaswa kushughulikiwa kwa pamoja.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako