Rais Xi Jinping wa China amesema, likiwa jukwaa muhimu la ushirikiano duniani, mfumo wa ushirikiano wa BRICS si kama tu unahusu nchi tano wanachama wake, bali pia unahusu matarajio ya nchi zote zinazoibuka kiuchumi, nchi zinazoendelea na jumuiya ya kimataifa. Alipohutubia ufunguzi wa kongamano wa viwanda na biashara kati ya nchi za BRICS, rais Xi alisema tunapaswa kupanua wigo wa ushirikiano wa BRICS ili nchi nyingi zaidi zinufaike, kwa kupitia kuanzisha mtandao wa kiwenzi, nchi nyingine zinazoendelea na zile zinazoibuka kiuchumi zinaweza kujiunga na shughuli zetu za kunufaishana zenye ushirikiano na mshikamano, ili kupata mafanikio ya pamoja.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |