Kiongozi wa upinzani wa Kenya Bw. Raila Odinga ameikosoa tume ya uchaguzi ya Kenya, kwa kupanga tarehe 17 Oktoba kuwa tarehe ya kurudia uchaguzi wa rais, baada ya mahakama kuu ya Kenya kufuta matokeo hayo na kutaka uchaguzi wa rais ufanyike upya.
Bw. Odinga amesema muungano anaouongoza wa NASA na wadau wengine hawakuhusishwa kwenye kupanga tarehe hiyo mpya. Bw. Odinga amesema uchaguzi hautaweza kufanyika katika siku hiyo, hadi matakwa yao yatakapotimizwa. Amesema wanataka kuwa na mchakato wa uchaguzi ulio wazi kikamilifu na wenye uwajibikaji.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |