Shirika la afya duniani WHO limetahadharisha kuhusu uwezekano wa kutokea kwa mlipuko wa ugonjwa wa malaria nchini Sudan Kusini. Tahadhari hiyo imetolewa wakati nchi hiyo inashuhudia wimbi kubwa la wakimbizi wa ndani, na msukosuko wa chakula kutokana na mapigano yaliyoanza mwishoni mwa mwaka 2013. WHO inakadiria kuwa watu milioni 1.3 wameugua malaria mwaka huu, huku maelfu wengine wakiathiriwa na kipindupindu na surua, haswa kwenye maeneo ya mto Nile na katika kambi za wakimbizi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |