Manchester City imeirarua bila huruma Liverpool kwa magoli 5-0 katika mchezo wa ligi kuu ya Uingereza na kufanikiwa kukwea nafasi ya kwanza ya msimamo wa ligi hiyo.
Kwingineko, Chelsea wameifunga Leicester City goli 2-1, nao Arsenal wakiona mwezi baada ya kuichaganga Bournemouth jumla ya magoli 3-0. Stoke City yenyewe imewabana mbavu Manchester United kwa kutoka sare ya goli 2-2. Na Tottenham ikiifunga Everton magoli 3-0.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |