Kiungo wa Simba Sports Club na timu ya Taifa ya Tanzania Said Ndemla, ameitwa nchini Sweden kucheza soka la kulipwa. Meneja wa mchezaji huyo Jamal Kisongo amethibitisha kuwa, mchezaji huyo alifuzu majaribio na sasa wako kwenye mchakato wa kupata visa kwa msaada wa TFF na serikali ili mchezaji huyo aweze kupata vibali na kwenda nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |