Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limepitisha uamuzi wa kuweka vikwazo vipya dhidi ya Korea Kaskazini kutokana na majaribio yake ya nyuklia yaliyofanyika tarehe 3 Septemba.
Uamuzi huo ukiwa ni wa tatu wa baraza hilo kuhusu Korea Kaskazini ndani ya wiki tano, unazuia karibu asilimia 30 ya utoaji wa mafuta kwake na kuzuia uuzaji wake wa vitambaa wenye thamani ya dola za kimarekani milioni 800 na kuwazuia wafanyakazi wa Korea Kaskazini kutuma fedha nyumbani kutoka nchi za nje.
Kwa mujibu wa vikwazo hivyo, asilimia 90 ya uuzaji nje wa Korea Kaskazini umezuiliwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |