• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Waziri wa mambo ya nje wa Sudan kutembelea Marekani

    (GMT+08:00) 2017-09-13 10:07:19
    Waziri wa mambo ya nje wa Sudan Bw. Ibrahim Ghandour leo anafanya ziara nchini Marekani ambako atajadili masuala yanayofuatiliwa kwa pamoja na pande hizo mbili, wiki nne kabla ya Marekani kufanya uamuzi kama itaondoa kabisa vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Sudan.

    Msemaji wa Wizara ya mambo ya nje ya Sudan amesema kwenye taarifa yake kuwa, Bw. Ghandour pia ataongoza ujumbe wa Sudan kuhudhuria Mkutano wa 72 wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa.

    Waziri wa mambo ya nje wa Sudan anatarajiwa kukutana na waziri wa mambo ya nje wa Marekani Bw. Rex Tillerson na maofisa wengine waandamizi.

    Mwishoni mwa mwezi Julai, Marekani ilirefusha kwa miezi mitatu muda wa kupitia uamuzi wake kama itaondoa kabisa vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Sudan vilivyowekwa kutokana na rekodi ya haki za binadamu ya nchi hiyo na masuala mengine.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako