Rais Bashar al Assad wa Syria amekutana na waziri wa ulinzi wa Russia Sergey Shoigu mjini Damascus, na kujadiliana kuhusu mpango wa ushirikiano wa majeshi ya nchi hizo mbili.
Bw. Shoigu amepongeza mafanikio yaliyopatikana na jeshi la Syria katika kuvunja udhibiti wa miaka mitatu wa kundi la IS katika jimbo la Dyerzur, mashariki mwa nchi hiyo.
Pande hizo mbili zimesisitiza tena msimamo wa kudumu wa kupambana na ugaidi nchini Syria hadi kuuondoa kikamilifu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |