• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • IGAD yafanya juhudi kuhimiza biashara huria na uhuru wa kusafiri kabla ya mwisho wa mwaka huu

    (GMT+08:00) 2017-09-14 10:17:45

    Shirika la maendeleo la kiserikali ya nchi za Afrika Mashariki IGAD linafanya juhudi kutimiza biashara huria na uhuru wa kusafiri kati ya nchi saba wanachama kabla ya mwisho wa mwaka huu.

    Akiongea kwenye mkutano juu ya itifaki ya IGAD kuhusu mawasiliano huru ya watu kwenye kanda hiyo, mkurugenzi wa Ofisi ya IGAD Kusini mwa Sudan Bw. Abdelrahim Ahmed Khalil alisema IGAD imeanza kujadiliana na nchi zote wanachama ili kuhakikisha itifaki hiyo inapitishwa kabla ya mwisho wa mwaka huu.

    Bw. Khalil amesema lengo la itifaki hiyo ni kuhimiza kiasi kikubwa cha shughuli zilizo nje ya taratibu kati ya nchi za IGAD kufanyika kwa kufuata kanuni halisi, na kuongeza fursa za mawasiliano halali.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako