Takwimu zilizotolewa na idara ya mambo ya bandari ya Kenya zimeonyesha kuwa, idadi ya bidhaa zilizopita kwenye bandari ya Mombasa katika miezi 7 ya mwanzo ya mwaka huu imeongeza kwa asilimia 11.9 ikilinganishwa na mwaka jana.
Idara hiyo imesema, katika kipindi hicho, bandari ya Mombasa imepitisha tani milioni 17.5 za bidhaa, na idadi ya kusafiri nje ya bandari hiyo imeongeza kwa asilimia 1.7.
Habari zinasema, kutokana na kukamilika kwa ujenzi wa reli ya SGR iliyojengwa na kampuni ya China, bandari hiyo inatarajia kupitisha bidhaa nyingi zaidi katika siku za baadaye.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |