Watu 120 wamethibitishwa kufariki dunia kutokana na tetemeko la ardhi lenye nguvu ya 7.1 kwenye kipimo cha Richter lililotokea jana alasiri katika jimbo la Morelos, katikati mwa Mexico. Kwa mujibu wa idara ya tetemeko la ardhi ya Mexico, hivi sasa kazi ya uokoaji bado inaendelea, na idadi ya vifo huenda ikaongezeka. Hii ni tetemeko kubwa la pili kuikumba Mexico katika wiki mbili zilizopita, na watu 98 walifariki dunia katika tetemeko lenye nguvu ya 8.2 lililotokea Septemba 7 nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |