• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • FIFA yaanza kuichunguza Chelsea kwa kukiuka sharia za usajili

    (GMT+08:00) 2017-09-21 08:23:23

    Kwa mara ya 8 klabu ya Chelsea imeingia matatani tena na shirikisho la soka duniani FIFA kutokana na kukiuka sheria za usajili wa wachezaji vijana, na sasa FIFA wameanza rasmi uchunguzi wao.

    Haijafahamika wazi ni wapi Chelsea wameonekana kukiuka sheria za usajili kwa wachezaji vijana lakini taarifa kutoka FIFA zimethibitisha kwamba wanaanza kufanya uchunguzi kuhusiana na klabu hiyo.

    Msemaji wa FIFA alipoulizwa kuhusiana na hili la kuichunguza Chelsea amekiri kwamba upelelezi unaendelea dhidi ya klabu hiyo lakini akakataa kuweka wazi kwamba nini haswa Chelsea wamefanya.

    Haijafahamika bado ni adhabu gani Chelsea watapewa wakikutwa na hatia lakini kosa walilofanya wao sio kubwa kama la Athletico Madrid na ni wazi hawatapewa adhabu kubwa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako