• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • China yazitaka pande mbalimbali za Peninsula ya Korea zijizuie

    (GMT+08:00) 2017-09-23 18:06:25
    Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Bw. Lu Kang jana amesema, hivi sasa hali ya peninsula ya Korea ina utatanishi, na pande husika zinapaswa kujizuia, na kufanya juhudi ili kupunguza hali ya wasiwasi, na si kuchocheana. Vilevile amesema China inapinga Korea Kaskazini kuendeleza silaha za kinyukilia, na msimamo huo ni wazi.

    Ikulu ya Marekani imetoa taarifa kuhusu mazungumzo kati ya marais wa Marekani na Korea Kusini yaliyofanyika Alhamisi kuwa, marais hao wawili walisisitiza kuwa nchi hizo mbili zinatafuta kwa pamoja njia ya kuihimiza Korea Kaskazini iache silaha za kinyukilia kwa njia ya amani. Pia wanaona kuwa, ili kuizuia Korea Kaskazini kuchukua hatua za kutishia na kuihimiza iache silaha za kinyukilia, ni lazima kuiwekea vikwazo kadiri iwezekanavyo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako