Banki Kuu ya Kenya iko katika hatua za mwisho za kuweka alama za usalama katika sarafu mpya, Hazina ya Taifa imethibitisha.
Uthibitisho huu umekuja baada ya uvumi kuenea kwenye mitandao ya kijamii wiki iliyopita vile pesa mpya itakuwa ikifanana.
Akizungumzia na wanahabari, Gavana wa Benki kuu ya Kenya amesema utoaji wa sarafu mpya utafanyika kwa mujibu wa Sheria ya Benki Kuu na sheria nyingine zinazoongoza mchakato.
Mwezi Machi mwaka jana, Gavana Njoroge alisema nia yao ya utoaji wa sarafu mpya ni kabla ya mwisho wa Septemba mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |