Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger ameilalamikia ratiba ya ligi kuu ya England kuwa haimtendei haki wakati huu ambapo timu ina mechi za michuano ya ligi ya mabingwa barani ulaya.
Wenger amesema ratiba hairuhusu wachezaji kupumzika hali ambayo inaweza kusababisha timu yake kufanya vibaya. Arsenal imecheza mechi ya EPL juzi jumatatu na kesho Alhamisi inatarajia kucheza katika michuano ya ligi ya mabingwa ulaya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |