Mwanamasumbwi, Ricky Burns ametamba kumpiga mpinzani wake Anthony Crolla katika mchezo unaotarajiwa kuchezwa Jumamosi hii. Pambano hilo la uzito wa lightweight litakalo fanyika Manchester Arena, Burns anaamini atawafurahisha mashabiki wake wakati atakapochukua ushindi mbele ya bingwa huyo wa zamani wa dunia. Mabondia wengi wamekuwa wakitamba kabla ya pambano lakini mwisho wake hupoteza mchezo.
Mabondia hao wote wawili wamepoteza mapambano yao ya mwisho kabla ya kukutana katika ulingo Jumamosi hii.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |