Idadi ya watu waliofariki katika ajali ya mashua iliyobeba Warohingya wanaotoka Myanmar kuelekea Bangladesh imefikia 12, na wengine kadhaa bado hawajulikani walipo.
Polisi nchini Bangladesh imesema, miili ya watu 12 imepatikana, wakiwemo watoto 10, mwanaume mmoja na mwanamke mmoja.
Polisi wamekadiria kuwa idadi ya vifo itaendelea kuongezeka, na kikosi cha ulinzi wa pwani na kikosi cha mpakani vitaendelea kufanya uokoaji katika eneo la ajali hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |